Kwa mujibu wa shirika la habari "Abna" kwa kunukuu Al Jazeera, Israel Katz, Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni, leo wakati wa ziara yake katika maeneo ya Syria alitangaza kwamba jeshi la utawala huo halitaondoka katika kile wanachokiita eneo lao la buffer kusini mwa Syria.
Alidai: "Hatutahama kutoka Mlima Hermon (Jabal al-Sheikh) na eneo la usalama mradi tu tishio dhidi ya Israel lipo. Ujumbe kwa Rais wa Syria ni wazi – unapoamka asubuhi kwenye ikulu ya Damascus na kutazama Mlima Hermon (Jabal al-Sheikh) na kuona jeshi la Israel, unajua kwamba tuko hapa kulinda jamii zetu na mipaka yetu."
Katz, akirejelea shambulio la wiki iliyopita kwenye kambi ya anga ya Syria, aliongeza kwamba Israel ilichukua hatua dhidi ya majaribio ya Uturuki kujipanga nchini Syria ambayo yanaweka katika hatari maslahi ya usalama ya Israel. "Tumeliweka hili wazi na tutashikamana nalo katika siku zijazo," alisema.
Maoni yako